Thursday, December 19, 2013

D"BANJ KUWEKEZA KWENYE KILIMO 2014.



 dbanj farming
Msanii kutoka  Nigeria Oladapo Oyebanjo aka Dbanji wakati akitarajia kusherehekea kutimiza miaka 10 tangu aanze kufanya music hapo  mwakani 2014 amejipanga kuingia katika shughuli za kilimo . 

 
Dbanj alianza  kufanya music 2004  ,kwa miaka 9 iliopita amepata pata mafanikio ikiwemo kupata tuzo ndani na nje ya Nigeria.
Sasa jamaa mwakani anampango wa kuwekeza katika kilimo ikiwa ni sehemu ya mafanikio anayoendelea kuyapata.
 dbanj agriculture
January 2014 Dbanj anatarajia kuhudhuria kongamano African Union Summit nchini Ethiopia ambapo ataingia makubaliano ya kuhamasisha kilimo cha wakulima wadogowadogo barani Africa.
 dbanj agriculture
Katika picha Dbanj anaonekana akifanya maandalizi ya kuwekeza katika kilimo

0 comments: