Saturday, June 07, 2014

Msanii wa kundi la Cali Swag District afariki dunia ..


Kuni la muziki kutoka  Marekani  Cali Swag District limempoteza memba wa kundi hilo  JayAre ambaye amefariki jana ijumaa ,

Kwa mujibu wa MTV News Cheron Childs  AkA JayAre amefariki kutokana na kusumbuliwa na sickle cell anemia  ambapo siku ya alhamisi alikimbizwa hospital lakini madaktari walishindwa kuokoa uhai wake.
Rafiki yake wa karibu ambaye walikuwa katika kundi moja la Cali Swag District (CSD) Smoove Da General alitweet kuhusu kifo cha Msanii huyo
 “Sickle cell took my brother away from me today…with that being said I’m proud to know that with that disease he made the best of his life,”
“Rest in peace Jayare I’m gonna miss u forever ..I will never get over this..but I know God got u..and I know You got me.”
Kundi hilo lilianza likiwa na wasanii wanne hivi sasa limebakia na wasanii wawili  kwani JayAre sio msanii wa kwanza wa kundi la  Cali Swag District kupoteza maisha akiwa na umri mdogo , May 2011, Montae “M-Bone” Talbert msanii mwingine kutoka katika kundi hilo alifariki dunia kwa kupigwa risasi.
Kundi hili la Cali Swag District  lilipata umaarufu mwaka 2010 kupitia wimbo wao uliuza platinum “Teach Me How to Dougie” wimbo ulikuepo kwenye albam yao ya kwanza The Kickback. Mwanzoni mwa mwaka huu walitoa Mixtape The District wakiwa wamewashirikisha Nipsey Hussle, Ty Dolla $ign, na Waka Flocka Flame.

0 comments: