Thursday, December 27, 2012

Chris Brown anajua kuwapanga Karuache Tran na Rihanna! Baada ya kula bata na Karuache kule Paris,Christmas hii alikuwa na Rihanna Los Angeles...


Pamoja na kwamba mpaka sasa Chris Brown na Rihanna hawakubali  kuwa wao ni couples lakini matukio ya kuthibitisha hili yanazidi kuonekana.
Jana (december 25) katika kusheherekea sikukuu ya Christmas star kutoka Barbados Rihanna mwenye miaka 24 aliamua kuchukua flight hadi Los Angeles ambako ali-join na Chris Brown kushuhudia mechi ya mpira wa kikapu baina ya Lakers na Knicks iliyopigwa katika uwanja wa Staples Center, Los Angeles  Marekani.
Ni kama wametoa picha yenye maelezo kuwa wameamua kurudiana tena na kuendelea na maisha yao pamoja, na hii ni baada ya Chris Brown kuonekana kuvuruga makubaliano yao hivi karibuni na kula bata na mpenzi wake wa zamani Karuache Tran huko Paris Ufaransa, kitu ambacho kilimkera sana Rihanna na kuandika tweet za matusi ambazo zilionekana kabisa kuwa zilielekezwa kwa Chris Breezy kwa kukutana tena na Karrueche Tran wakati huo Rihanna yuko mpweke kwenye mapumziko yake akitegemea ujio wa Chris Brown.
Chris Brown na RiRi walionekana wenye furaha sana wakitabasamu na kucheka mara kwa mara wakati wanaangalia mechi ya Lakers siku hiyo ya Christmas huko Los Angeles. Ni kama Chris Brown anaweza kuwamudu na kuwacontrol warembo hawa wawili matata.

Baada ya game kuisha RiRi alitweet picha aliyopiga na Chris Brown wakiwa wamepose katika Porshe 911 Turbo S aliyozawadiwa na lebel yake ya Roc Nation ya mtu mzima Jay Z hivi karibuni, na picha hiyo ilikuwa na caption iliyosomeka "Thug Life, Merry Christmas".
 
 
 


 
 

0 comments: