Tuesday, October 30, 2012

Akon amsaini Konvict mtoto wa mtaani kutoka kenya mwenye miaka 14, story yao ni kama movie. ..



Wiki hii imeanza na zali zaidi ya lile la mentali kwa mtoto ambae alikuwa anaishi katika mazingira magumu sana nchini Kenya, inaweza kuwa ni ndoto aliyoota imekuwa kweli na kama hakuwahi kuota basi Mungu amemsapraiz na kujikuta anapata deal la uhakika la kufanya muziki chini ya lebel kubwa duniani ya ‘Konvict Muzik’
Mtoto huyo Wilson alimsimamisha Akon jijini Nairobi juzi wakati anaelekea kupiga show katika ukumbi wa Nairobi Carnival na akaona kabisa kuwa hii ilikuwa ni chance ya yeye kumueleza Akon ya moyoni na sio kumuomba mkwanja kama wafanyavyo wengine…ila ni kumuomba kujiunga na lebel ya Konvict. Duh, unaweza kudhani mtoto huyo alikuwa mwehu eeeh…dogo alirusha mkuki vizuri!!
Baada ya Akon kukubali kusimama tu mtoto huyo alizitumia dakika chache kumsimulia hali mbaya ya maisha aliyonayo na jinsi ambavyo baba yake alivyomtesa na kulazimika kulala nje, akaeleza jinsi gani anavyoupenda muziki na hana jinsi ya kuweza kuingia studio kurekodi. Surprisingly, Akon akaamua kumpa nafasi, akaruhusu aingizwe kwenye gari lake na wakaelekea wote kwenye concert yake.
Hatujui nini kiliendelea kwenye gari lakini inaonekana waliendelea kuongea kuhusu yale waliyoyaanzisha. Na haikuwa rahisi kwa Akon kumpa nafasi kirahisirahisi tu.
Wakati anaendelea na performance yake mkali huyo toka Senegal alimuita stejini yule dogo. Kwa mara ya kwanza kwenye jukwaa kubwa kama lile…Akon akamkabidhi dogo mic na kumwambia aperform!
Ni kama ulikuwa mtihani wa mwisho kwa dogo huyo ambao ungemtoa lawama Akon kirahisi, dogo alifunika vibaya na kuonesha kipaji kikubwa alichonacho.
Haikuhitaji press release ama press conference kutangaza uamuzi…Akon alichokifanya alishika mic na kutangaza mbele ya umati wa watu, “Wilson the newest member of the Konvict family”. Ni hivyo tu dogo anachukua pipa kwenda kuishi ndoto zake Marekani.
Huyu ni mtoto wa kiafrika mwenye story ya mafanikio inayofanana na ya Akon.

0 comments: