Thursday, August 01, 2013

Uruguay kuhalalisha utumizi wa Bangi


Bangi

Bunge la Uruguay limepitisha mswada wa kuhalalisha bangi. Ikiwa mswada huu utapitishwa na Baraza la Senate, Uruguay itakuwa nchi ya kwanza kuhalalisha uzalishaji na utumiaji wa bangi.
Hatua hii inaungwa mkono na serikali ikisema itapunguza mapato na faida kubwa kwa walanguzi wa mihadarati pamoja na kuwafanya watumizi wa bangi kutotumia dawa kali za kulevya.Chini ya mswada huo ni serikali pekee itakua na kibali cha kuuza bangi..


Pia serikali itatoa utaratibu wa uzalishaji, mavuno,
uhifadhi na mauazo ya nje. Wanunuzi wote watanakiliwa kwenye daftari maalum na sharti wawe wametimiza miaka 18 na zaidi. Mteja anaweza tu kununua kilo 40 kwa mwezi kutoka kwa maduka ya dawa au kukuza mimea sita ya bangi.Wageni hawatakubaliwa kununua bidhaa hii.
Wabunge 50 kati ya 96 walipitisha mswada huo. Wanaotetea kuhalalishwa kwa bangi wamesema vita dhidi ya mihadarati havijapiga hatua na ipo haja kuweka mbinu mpya.
Kwa miongo mingi kanda ya Latin America imekumbwa na ghasia za magenge ya mihadarati ambapo maelfu ya watu wamekufa. Matukio ya Uruguay yanatazamwa kwa karibu eneo hilo ikiwa yatasaidia kupunguza machafuko yanayotishia uthabiti wa mataifa mengi.
BBC Swahili

0 comments: