Tuesday, July 30, 2013

kambi ya vijana ( IYF 2013 world camp tanzania ) yazinduliwa leo Dar



Dkt,Mh. Fenella Mukangara  

NA Godwin Mmari
Waziri wa habari vijana, tamaduni na michezo Dkt,Mh. Fenella Mukangara amezindua rasmi kambi ya vijana kutoka mikoa na nchi mbalimbali jijini Dar es salaam ijulikanayo kama IYF 2013 WORD CAMP TANZANIA.

Katika uzinduzi huo Mh. Fenella amesema kuwa wazazi/walezi wanajukumu na wajibu wa kukabiliana na changamoto za vijana katika kubadilisha fikra hasi na kuwa na fikra chanya zitakazojenga nchi yetu.

                                    Band kutoka korea ikitumbuiza nyimbo za kitanzania
wanafunzi kutoka chuo cha biashara IFM wanaoshiriki katika kambi hiyo.

Kambi hiyo ya vijana iliyochukua vijana mbalimbali duniani imezinduliwa leo ambapo ilianza rasmi tarehe 29, July mpaka tarehe 3, Augost 2013 ambapo kutakuwa na michezo mbalimbali ya kitaifa na kimataifa kwa lengo la kuweka vijana na kutokomeza fikra hasi na kuwa na fikra chanya, yenye kauli mbiu ‘’BADILISHA FIKRA’’
                               wanataikwondo kutoka Kenya wakionesha umahiri wako katika mchezo huo

 waandishi wa habari wakibadilishana mawazo

0 comments: